ZIZA BAFANA ADAI ANGUKO LAKE KIMUZIKI LIMETOKANA NA UCHAWI

You are currently viewing ZIZA BAFANA ADAI ANGUKO LAKE KIMUZIKI LIMETOKANA NA UCHAWI
  • Post category:Burudani

Msanii wa muziki kutoka Uganda Ziza Bafana ni moja kati ya wasanii tajika nchini humo na amekuwa kwenye muziki kwa miaka kadhaa sasa kabla ya kupotea kwenye game baada ya kubadilisha menejimenti yake iliyokuwa ikisimamia kazi zake.

Kutokana na kutofanya vizuri kwenye muziki Ziza Bafana alihamua kujiingiza kwenye matumizi ya dawa  za kulevya ili aweze kusahau masaibu yaliyokuwa yakimsibu.

Sasa akiwa kwenye moja ya interview Mkali huyo wa ngoma ya akalulu amedai kuwa anguko lake kimuziki lilisababishwa na uchawi aliofanyiwa na wasanii wenzake.

Ziza Bafana ameenda mbali zaidi na kusema kwamba wasanii wengi nchini uganda wanatumia nguvu za giza kuwazima wasanii wanaofanya vizuri kwenye muziki nchini humo,hivyo amekiri kuwa  mmoja wa waathiriwa wa uchawi.

Hata hivyo wadau wa muziki wanahoji kwamba matatizo ya ziza bafana yametokana na uraibu wa madawa ya kulevya, hivyo amekuwa akiishi maisha ya uchochole tangu hatengane na aliyekuwa meneja wake Roger Lubega.  

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa