MSANII SOPHIA GOMBYA AFUNGUKA KUHUSU UTOFAUTI ULIOPO KATI YAKE NA YKEE BENDA.

You are currently viewing MSANII SOPHIA GOMBYA AFUNGUKA KUHUSU UTOFAUTI ULIOPO KATI YAKE NA YKEE BENDA.
  • Post category:Burudani

Mwanamuziki wa bendi nchini Uganda Sophia Gombya amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu utofauti kati yake na msanii ykee benda.

Akipiga stori na runinga ya NBS Gombya amesema Ykee Benda ni mtu wa wivu ambaye uhisi vibaya pindi wasanii wengine nchini Uganda wakimtambua kama rais wa muungano wa wanamuziki nchini humo.

Aidha amesisitiza kuwa hana ugomvi wowote na mkali huyo wa ngoma ya “Eva” huku akisema kwamba huwa anaumia sana wanamuziki wengine wakimvunjia Ykee Benda heshima lakini pia amekiri kuwa sio makosa yake watu wanapomuita rais wa muungano huo.

Ikumbukwe Sophia Gombya alijuzulu mwishoni mwa mwaka wa 2020 kama rais wa muuungano wa wanamuziki nchini Uganda wadhfa ambao Ykee Benda aliuchukua lakini baada ya miezi kadhaa alijiondoa kwa madai kwamba wasanii wengi nchini humo wanamdharau.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa