WIMBO WA DAVIDO UITWAO “IF” WAFIKIA MAUZO YA GOLD NCHINI MAREKANI

You are currently viewing WIMBO WA DAVIDO UITWAO “IF” WAFIKIA MAUZO YA GOLD NCHINI MAREKANI
  • Post category:Burudani

Ikiwa tayari ni miaka minne imepita tangu nyota wa muziki kutoka nchini Nigeria, Davido aachie hit song yake iitwayo “IF”, good news ni kwamba hadi kufikia sasa ngoma hiyo tayari imeshagonga Gold kwenye mauzo yake sokoni, yaani imeuza nakala zaidi ya laki tano kwa Marekani.

Kutokana na hatua hiyo chama cha Recording Industry Association of America (RIAA) kimetoa taarifa hiyo kupitia tovuti yake huku ikisubiriwa Davido kukabidhiwa cheti chake.

“IF” umeweka rekodi ya kuwa wimbo wa pili wa mahadhi ya Afro beat ulioimbwa na msanii mmoja (Solo song) kufikisha kiwango hicho cha mauzo kwa Marekani.

Haya hivyo, “IF” unakua wimbo wa pili kwa Davido baada ya “FALL” ambao nao ulifikia kiwango cha mauzo ya Gold, Mei 28, 2020.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa