Mwanamuziki wa kundi la Goodlife Crew, Weasel Manizo hataki mchezo linapokuja suala la wanawake.
Amewahakikishia wale ambao mara nyingi humlinganisha na mwanamuziki wa Bongofleva Diamond Platinumz kuwa hakuna anayemshinda kwenye masuala ya wanawake.
Akizungumzia ishu ya Diamond kurudiana na baby mama wake Tanasha Donna, Weasel amesema kuwa yeye amekuwa akiwaunganisha wanawake wote aliopata nao watoto kama namna ambavyo mkali huyo wa Bongofleva amekuwa akifanya bila kuweka hadharani.
Hata hivyo mkali huyo wa muziki kutoka nchini Uganda amewashauri wanaume wote ambao wamezaa na wanawake wengi kuhakikisha kwamba wanawaleta pamoja badala ya kuwakimbia.
Ikumbukwe Weasel Manizo anadai kuwa na zaidi ya watoto 20 aliopata na wanawake tofauti.