Wakulima wa mahindi Kaskazini mwa Bonde la Ufa wameshtumu hatua ya Bodi ya Kitaifa ya Mazao na Nafaka NCPB kupunguza bei ya mahindi kwa gunia la kilo tisini hadi shilingi alfu mbili mia tano.
Wakulima hao kwa sasa wanatoa wito kwa serikali kuangazia malilio yao kwani bei hiyo ni ya chini mno ikilinganishwa na gharama ya uzalishaji.
Yanajiri hayo huku mbunge wa Moiben ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo Bungeni Sila Tiren akisema hatua ya NCPB kushusha bei inahujumu juhudi zilizopigwa katika kutatua matatizo ya wakulima.