WAKULIMA WADOGO WADOGO NCHINI KUTAFUTA SOKO YA MAZAO YAO NCHINI CHINA.

You are currently viewing WAKULIMA WADOGO WADOGO NCHINI KUTAFUTA SOKO YA MAZAO YAO NCHINI CHINA.
  • Post category:Biashara

Wakulima wadogo wadogo nchini  wananuia kupanua mauzo yao kwenda kwa soko la Uchina ili kupata faida zaidi.

Mkurugenzi  mkuu wa muungano wa wakulima wadogo wadogo Justus Lavi Mwololo anasema kuwa masoko ambayo Kenya hupeleka bidhaa zake kama vile Marekani na Ulaya,yanakabiliwa na changamoto kutokana na vizuizi vya kibiashara vilivyowekwa ili kudhibiti msambao wa virusi vya COVID-19.

Kulingana na  Mwololo ,China imeweza kukabiliana na janga la COVID-19  huku ikifungua tena soko lake kwa uagizaji  wa bidhaa kutoka nje na hivyo ni fursa nzuri kwa wakulima wa maembe, parachichi na bidhaa nyingine za kilimo.

Mwololo ameongeza kuwa taifa hilo la Afrika Mashariki limekuwa likiuza kiasi kidogo tu cha mazao yake ya kilimo nchini China lakini sasa wakulima wadogo wanapanga kuongeza.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa