WAKENYA WAONYWA DHIDI YA KUTAPELIWA KUPATA HUDUMA NAMBA.

You are currently viewing WAKENYA WAONYWA DHIDI YA  KUTAPELIWA KUPATA HUDUMA NAMBA.

Msemaji wa serikali kanali mstaafu Cyrus Oguna amewaonya wakenya dhidi ya kutapeliwa kulipia ada ili kupata kadi zao za huduma namba kwani hakuna ada yoyote inayotozwa wananchi kupokea kadi hizo.

Oguna amesema zoezi la kusambaza kadi hizo imeanza rasmi ambapo watu wazima watakabidhiwa kadi hizo huku watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane wakipewa nambari maalum.

Aidha amedokeza kuwa watu 37,000 walisajiliwa katika awamu ya kwanza ya mpango wa huduma namba huku wengine wakitarajiwa kusajiliwa mwezi Aprili mwaka huu.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa