RAIS KENYATTA AZINDUA ZOEZI LA KUSAMBAZA CHANJO YA COVID-19 KOTE NCHINI.

You are currently viewing RAIS KENYATTA AZINDUA ZOEZI LA KUSAMBAZA CHANJO YA COVID-19 KOTE NCHINI.

Rais Uhuru Kenyata mapema leo amezindua rasmi shughuli ya usambazaji wa chanjo dhidi ya virusi vya Corona hadi katika maeneo mbalimbali nchini

Akizungunza katika eneo la Kitengela ambapo chanjo hiyo imehifadhiwa rais Kenyata anasema ana imani kwamba wakenya wote watapata chanjo hiyo kusaidia kukabili ugonjwa wa COVID-19.

Aidha kiongozi wa taifa amewaonya  Wakenya dhidi ya kupuuza masharti yaliyowekwa huku akiwataka kuendelea kuchukua tahadhari ili kuepuka Corona.

Kwa upande wake waziri wa Afya Mutahi  Kagwe anasema  uwepo wa chanjo hiyo hapa nchini ni hatua kubwa ikizingatiwa kwamba Kenya ni miongoni mwa mataifa ya kwanza barani afrika kupata chanjo ya kubali Corona.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa