Kundi la muziki wa Hiphop nchini Wakadinali limeachia rasmi album yao mpya iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki wao.
Album hiyo iitwayo “Victims of Madness” ina jumla ya ngoma 15 za moto huku wakiwa wamewashirikisha wasanii kama Breeder, Abbas Kubaff na wengine kibao.
“Victims of Madness” ni album ya tatu ya Wakadinali baada ya “Ndani ya Cockpit” ya mwaka wa 2017 na “Mtoto wa Mama” ya mwaka wa 2019 na album hiyo inapatikana ‘Exclusive’ kupitia mitandao yote ya kukisikiliza na kupakua muziki duniani kama vile Boomplay,Spotify na Apple Music.