VISA YA MIMBA ZA MAPEMA VYAONGEZEKA KAUNTI NDOGO YA TURKANA

Kaunti ya ndogo ya Turkana ya Kati  imeripoti visa  1,282 vya mimba miongoni mwa wasichana walio na umri mdogo kati ya mwezi Machi na Juni mwaka huu.

Afisa wa kituo cha Huduma kwa Vijana  katika hospitali ya Rufaa ya Lodwar Virginia Ikal amesema kuwa hali hiyo inasababishwa na hatua ya kufungwa kwa shule kwa muda mrefu kutokana na athari za janga la virusi vya corona.

Aidha Ikal amesema baadhi ya wasichana walio na ujazito wana umri wa kati ya  miaka 10 na  19  huku akisema vijiji vya Kanamker,Nawoitorong na Nakwamekwei  vilivyoko viungani mwa mji wa Lodwar vimeripoti idadi ya juu ya wasichana waliopachikwa mimba wakiwa na umri mdogo.

Wakati  huo huo Mshauri katika kituo cha vijana  katika hospitali ya Rufaa ya Lodwar Bereta Onduu amewataka wazazi pamoja na washikadau kuwa mstari wa mbele katika kupiga vita kukithiri kwa mimba za mapema na kuwapa nasaha njema watoto wao

Hata hivyo amesema ni muhimu hatua za haraka kuchukuliwa ili kukomesha tabia hiyo ambayo aliitaja kama dhuluma  kwa  wasichana wadogo kwani wengi wao wameambukizwa magonjwa ya zinaa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa