VINKA ATHIBITISHA KUREJEA TENA KWENYE MUZIKI BAADA YA KUDAIWA KUCHUKUA LIKIZO YA ULEZI.

You are currently viewing VINKA ATHIBITISHA KUREJEA TENA KWENYE MUZIKI BAADA YA KUDAIWA KUCHUKUA LIKIZO YA ULEZI.
  • Post category:Burudani

Staa wa muziki kutoka nchini Uganda Vinka amedai kwamba likizo ya uzazi au ulezi haiwezi kumlisha hivyo amethibitisha kurejea tena kwenye shughuli zake za kimuziki.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Vinka amepost baadhi ya picha akiwa anatumbuiza kwenye hafla ya harusi na kuthibitisha kwamba ameanza kufanya matamasha mbali mbali ya muziki ili aweze kujikimu kimaisha.

Kauli Vinka inakuja wiki moja baada ya kupewa  likizo ya miezi sita kwa ajili kutoa malezi kwa mtoto wake lakini inaonekana amekaidi amri hiyo na kuanza kutumbuiza kwenye hafla mbali mbali ya harusi.

Ikumbukwe mwanamuziki huyo ambaye yupo chini ya lebo ya muziki ya Sony Music Entertainment hajeoneka mbele ya umma au kutumbuiza kwenye hafla yeyote kwa takriban mwaka mmoja.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa