UTANI WA LUPITA NYONG’O BAADA YA WAZIRI UTALII NCHINI KUSEMA WALIMTAFUTA KWA MIAKA 5

You are currently viewing UTANI WA LUPITA NYONG’O BAADA YA WAZIRI UTALII NCHINI KUSEMA WALIMTAFUTA KWA MIAKA 5
  • Post category:Burudani

Mara baada ya Naomi Campell kutangazwa kama balozi wa utalii nchini,wakenya wengi walihoji kwanini wizara ya utalii imchague Campell na sio muigizaji wa kimataifa Lupita Nyongo ambaye ana asili ya Kenya.

Waziri wa utalii nchini “Najib Balala” alijibu kwa kusema kuwa wizara yake ilijaribu kuwasiliana na Bi Nyong’o bila mafanikio kwa miaka mitano sasa.

Waziri Balala alisema “Najua kila mtu anajiuliza kwanini sio Lupita,Lupita anamakubaliano na menejimenti yake na mameneja wake hawakuturuhusu kumpata Lupita,ni kwa miaka mitano sasa tumekuwa tukimtafuta Lupita” hicho ndicho alichokisema Waziri Balala

Lupita Nyongo pia ameisikia kauli hii ya waziri na kuwaaminisha watu kuwa hakuwahi kutafutwa,alipost picha ambayo anacheka kwenye ukurasa wake wa Twitter na kuandika “Mimi ninaposikia kuwa waziri wa utalii amekuwa akinitafuta kwa miaka 5”.

Kwa post hiyo ya Lupita huenda hakuwahi kupata taarifa za yeye kutafutwa na wizara ya utalii nchini Kenya.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa