BABA LEVO AKANUSHA KUMSEMA HAMISA MOBETTO

You are currently viewing BABA LEVO AKANUSHA KUMSEMA HAMISA MOBETTO
  • Post category:Burudani

Msanii wa Bongo Fleva, Baba Levo amekanusha kuwa kauli yake haikumlenga Mwanamitindo na msanii Hamisa Mobetto kama inavyotafsiriwa na baadhi ya watu mtandaoni na Hamisa mwenyewe.

Baba Levo alipangua madai hayo na malalamiko yaliyotafsiriwa kumlenga Hamisa kupitia video yake ambayo ilianza kusambazwa mitandaoni anayosikika akisema ‘Misa’ anaweza kujifungua ‘Mbwa’.

Baada ya kusambaa kwa video hiyo, Hamisa kupitia Insta Story kwenye mtandao wa Instagram alishusha lawama za moja kwa moja kwa msanii huyo akionesha kutopendezwa na kauli hiyo ya Baba Levo.

Hata hivyo muda mchache baada ya lawama za Hamisa, Baba Levo kupitia akaunti yake ya Instagram alikanusha madai hayo na na kueleza kuwa hajamtaja Hamisa kama inavyotafsiriwa bali alisema ‘Misa’.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa