Rapa The Game amedai kwamba yeye ndiye rapa bora kutoka mji wa Compton ambao ni zao la wasanii wakali wa muziki wa hip hop nchini Marekani.
Kwenye mazungumzo yake hivi karibuni, The Game pamoja na washkaji zake walikuwa wakijadili ni nani rapa mkali kutoka kwenye mji huo, na The Game hakuacha kujipakulia misifa kwa kujitaja mwenyewe.
Japo liliibuka jina la rapa Kendrick Lamar na wengine kwenye mjadala huo kama rapa bora wa Compton, lakini The Game alisema anakubali anachokifanya Lamar kwenye muziki wa hiphop lakini yeye ni bora zaidi.