SPICE DIANA AFUNGUKA KUHUSU WAFUASI WA BOB WINE KUSUSIA MUZIKI WAKE.

You are currently viewing SPICE DIANA AFUNGUKA KUHUSU WAFUASI WA BOB WINE KUSUSIA MUZIKI WAKE.
  • Post category:Burudani

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Spice Diana amefunguka kwa mara ya kwanza tangu wafuasi wa Bob Wine watishia kususia muziki wake.

Hitmaker huyo wa ngoma ya Kokonya anaamini kuwa wapinzani wake wanafadhili watesi wake kwenye mitandao ya kijamii kuzima juhudi zake za kuupeleka muziki wake kwenye level nyingine.

Akipiga stori na radio moja nchini uganda spice diana amesema kuna ubinafsi mwingi miongoni mwa wasani  nchini uganda na wengi wamekuwa wakimpiga vita kuhakikisha anafeli kwenye muziki wake lakini amehapa kupambana nao kwa kutoa muziki mzuri.

Ikumbukwe mapema wiki iliyopita wafuasi wa bob wine walitishia kususia muziki wa Spice Diana baada ya msanii huyo kukaa kimya kuhusu ishu ya Bob Wine kufungiwa nyumbani kwake mara baada ya matokeo ya uchaguzi nchini Uganda kutangazwa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa