RUTO: KUBADILISHWA KWA KATIBA SIO SULUHU KWA MATATIZO YANAYOWAKABILI WAKENYA.

You are currently viewing RUTO: KUBADILISHWA KWA KATIBA SIO SULUHU KWA MATATIZO YANAYOWAKABILI WAKENYA.

Naibu wa rais William Ruto amesema tatizo kubwa linalolikumba taifa hili si kufanyia marakebisho katiba kupitia mswada wa BBI ila ni kusuluhisha matatizo yanayokikumba mkenya wa kawaida kumwezesha kujiimarisha kiuchumi.

Akihutubu kwenye eneo bunge la Endebess Ruto amesema mpango kama ule wa ajenda kuu nne ya serikali ndio utakaostawisha taifa hili

Aidha Ruto amewarai washindani wake kusitisha siasa za ukabila na badala yake kuangazia  sera za maendeleo kwa faida ya wananchi.

Kwa upande wake mwakilishi wa kike wa kaunti ya Trans-Nzoia, Janet Nangabo amemtaka  rais uhuru kenyatta kuwaadhibu mawaziri wanaoendeleza  siasa za  mirengo badala ya kutekeleza wajibu wao kwa mujibu wa katiba.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa