RAPA GNL ZAMBA AWATOLEA UVIVU WASANII WAPYA WA HIPHOP NCHINI UGANDA

You are currently viewing RAPA GNL ZAMBA AWATOLEA UVIVU WASANII WAPYA WA HIPHOP NCHINI UGANDA
  • Post category:Burudani

Msanii nguli wa muziki wa Hiphop kutoka Uganda GNL Zamba ameweka wazi kuwa hakuna rapa yoyote kwa sasa  nchini humo anayemfanya ashindwe kulala usiku akimsikiliza.

Akiwa kwenye moja ya Interview GNL Zamba ambaye vizuri na  wimbo wake uitwao “Saba Saba” amesema marapa wengi  nchini  Uganda wamepoteza uhalisia wa muziki wa hiphop kwani mashairi yao hayaendani na midundo ya nyimbo husika, jambo ambalo anadai imepelekea muziki wao kukosa mashiko.

GNL Zamba ambaye ni moja kati  ya wasanii nguli wa muziki wa hiphop nchini Uganda amekuwa akiwasifia wasanii Fefe Bussi, Navio, na Recho Ray huku kwa upande mwingine akionekana kuwarushia madongo wasanii Gravity Omuttujju na Victor Kamenyo ambao wamekuwa wakishandane nae kwenye muziki wa Hiphop.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa