RAPA GNL ZAMBA ATENGUA KAULI YAKE YA KUOA MKE WA PILI.

You are currently viewing RAPA GNL ZAMBA ATENGUA KAULI YAKE YA KUOA MKE WA PILI.
  • Post category:Burudani

Rapa kutoka nchini Uganda GNL Zamba aligonga vichwa vya habari vya burudani majuzi mara baada ya kutangaza kwamba anamtafuta mke wa pili  afunge nae ndoa.

Zamba kwenye interviews mbali alikiri kwamba mke wake Tamar ambaye ni raia wa nchini marekani alimpa ruhusa ya kumuoa mke wa pili kutoka Africa.

Sasa rapa huyo  kwenye moja ya Interview ametengua kauli yake hiyo ya kumuoa mke wa pili kwa kusema kwamba alikuwa anatania tu, hivyo watu wasichukulie jambo kwa ukubwa.

Hata hivyo GNL Zamba amewataka wanawake ambao wamekuwa wakimtumia picha zao kwenye mitandao yake ya kijamii kwa ajili ya kumshawishi wafunge nae ndoa wakome mara moja kwani anamheshimu mke wake.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa