BEBE COOL, JOSE CHAMELEONE NA BOB WINE WATAKIWA KUCHANGIA GHARAMA YA MATIBABU YA MSANII EVELYN LAGU.

You are currently viewing BEBE COOL, JOSE CHAMELEONE NA BOB WINE WATAKIWA KUCHANGIA GHARAMA YA MATIBABU YA MSANII EVELYN LAGU.
  • Post category:Burudani

Msanii wa kike nchini Uganda Evelyn Lagu amelazwa hosptilani kwa miaka mitatu sasa kutokana na matatizo ya figo.

Juzi kati alitangaza anahitaji kupandikiziwa figo ili aweze kuishi kwa muda mrefu na matibabu yake yatagharimu shillingi millioni 7.5.

Kutokana na hilo, hafla ya kuchangisha pesa ilifanyika wikiendi hii iliyopita jijini kampala ambapo shillingi laki 6 ilikusanywa kwa ajili ya kugharamia matibabu ya msanii huyo.

Sasa baadhi ya Mashabiki wa muziki nchini uganda wamewataka wasanii Jose Chameleone, Bebe Cool na Bob Wine wachangishe fedha za  kugharamia  matibabu ya msanii Evelyn lagu.

Hii ni baada ya wasanii hao kukosa kufika au kutuma wawakilishi wao kwenye hafla ya kuchangisha fedha za kugharamia matibabu ya evelyn lagu iliyofanyika Jiji Kampala licha ya wanamuziki hao kuwa matajiri.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa