RAPA DABABY AFUNGULIWA MASHTAKA KWA KOSA LA KUMPIGA NA KUMNG’OA MTU JINO.

You are currently viewing RAPA DABABY AFUNGULIWA MASHTAKA KWA KOSA LA KUMPIGA NA KUMNG’OA MTU JINO.
  • Post category:Burudani

Staa wa muziki wa Hiphop kutoka nchini Marekani DaBaby amefunguliwa mashtaka kwa kosa la kumpiga ngumi mwenye nyumba hadi kumtoa Jino. 

Rapa huyo alikodisha nyumba kwa ajili ya kufanyia video ya  wimbo wake, na walikubaliana na mwenye nyumba kuwaingiza watu 12 tu ndani kulingana na kanuni za COVID-19.

Kinyume na masharti, DaBaby aliingiza watu takribani 40, mwenye nyumba hiyo ambaye amefahamika kwa jina la Gary Pagar alipoamua kumfuata kwa kuvunja masharti ya mkataba, mtu mmoja kutoka kambi ya DaBaby alimvamia na kumuangusha chini.

Baada ya hapo DaBaby alitoka kwenye gari na kumkimbiza pagar hadi ndani ambapo alianza kwa kumuonya kutowapa taarifa polisi kisha alimtwanga ngumi ya uso hadi kumng’oa jino. Shuhuda mmoja alipiga simu kuita polisi, na DaBaby na timu yake walikimbia eneo hilo.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa