Baada ya rapa kutoka nchini Marekani Meek Mill kuomba shabiki zake kupitia mtandao wa twitter wamsaidie kuwatag wasanii wanaochipukia kutoka nchini Nigeria, Davido ameijibu tweet hiyo ya Meek Mill kwa utani.
Kupitia mtandao wa twitter Davido ameijibu tweet ya Meek Mill kwa kumwambia kwa utani kuwa “usituchezee nyimbo zinazofanya vizuri ndio sisi”.
Ikumbukwe Davido na Meek Mill walishawahi kufanya kazi ya pamoja iitwayo “Fans Me” iliyotoka mwaka wa 2015 na sasa huenda Meek Mill anahitaji ladha nyingine ya msanii kutoka Nigeria katika muziki wake au anahitaji kumsaini kwenye lebo yake ya Dream Chasers Records.