RAPA CARDI AKIRI KUWA CHINI YA SHINIKIZO KUIACHIA ALBUM YAKE MPYA.

You are currently viewing RAPA CARDI AKIRI KUWA CHINI YA SHINIKIZO KUIACHIA ALBUM YAKE MPYA.
  • Post category:Burudani

Mafanikio ya album yake ya kwanza ya ‘Invasion of Privacy’ bado yanamtesa rapa Cardi B kutoka nchini Marekani.

Rapa huyo amesema mpaka sasa amesharekodi jumla ya nyimbo 50 lakini bado hajaridhika kwani anapata hofu na hajui ni ngoma zipi ziingie kwenye album yake ya pili.

Ikumbukwe sio mara ya kwanza kwa rapa Cardi B kukiri kuwa yupo chini ya shinikizo kwani mwishoni mwa mwaka wa 2020 alidai kuwa na hofu na angekosa kutoa wimbo mkali tena, watu wangesema ameshindwa na muziki.

Hata hivyo kinyume na hofu yake, mwezi Agosti mwaka huo  aliachia mkwaju wake uitwao “WAP” aliomshirikiaha Megan Thee Stallion na mpaka sasa dunia inazungumza habari zake.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa