Rapa A.Y kutoka nchini Tanzania ametusanua kilichompeleka nchini Marekani.
Hii ni baada ya picha yake aliyopiga akiwa karibu na jengo la Interscope Records kuibua maswali mengi miongoni mwa mashabiki zake.
A.Y ambaye alianza kuonekana kwenye filamu ya “Girlfriend” mwaka wa 2003, ametupa GOOD NEWS kupitia ukurasa wake wa instagram kuwa alienda nchini marekani kufanya filamu na mmoja kati ya waigizaji wakongwe wa Hollywood, Robert Davi.
Robert Davi anafahamika kwa umahiri wake kwenye ulimwengu wa filamu tangu mwaka wa 1977 na miongoni mwa filamu maarufu alizocheza ni, Game of Death, The Butcher, na nyingine nyingi.