WASHIKADAU WA MASUALA YA WATOTO POKOT MAGHARIBI WATAKA MSWAADA WA MWAKA WA 2018 KUHUSU WATOTO KUPASISHWA KUWA SHERIA

Ni vema mswada kuhusu watoto mwaka 2018 kutekelezwa kwa vitendo na kuwa sheria ili kuweka uzito na uhai kwa masuala yanayohusu mtoto.

Ndio wito wa watoto gatuzi la Pokot Magharibi katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto Mwafrika chini ya usimamizi wa mashirika ya Declairs, DSW, SIKOM na Idara ya Watoto chini ya Serikali kuu.

Katika mazungumzo na North Rift Radio Gavana wa watoto kaunti hiyo Mercyline Chebet amesisitiza umuhimu wa kupasishwa kwa mswada wa mwaka 2018 kuwa sheria ili kumpa mtoto sauti kando na kumuepusha na dhuluma.

Ni kuali ambayo imechachawizwa na Moses Kibet ambaye amependekeza viongozi kutilia maanani masuala ya watoto kuliko siasa ambazo hazina uzito kwenye mizani ya ukuwaji wa jamii yenye maadili na siha njema.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa