OTILE BROWN NA DR. EDDIE WAMALIZA TOFAUTI ZAO BAADA YA KUWA KWENYE BIFU KWA MUDA.

You are currently viewing OTILE BROWN NA DR. EDDIE WAMALIZA TOFAUTI ZAO BAADA YA KUWA KWENYE BIFU KWA MUDA.
  • Post category:Burudani

Nyota wa muziki nchini Otile Brown na aliyekuwa meneja wake Dr. Eddie wamemaliza tofauti zao  baada ya kutokuwa na maelewano mazuri kwa muda.

Taarifa hizo zimethibitishwa na Dr. Eddie kupitia ukurasa wake wa Instagram baada ya kupost kipande cha video wakiwa location na Otile Brown na kuthibitisha kwamba wanatayarisha video mpya ya msanii huyo.

Dr. Eddie alienda mbali zaidi na kusema kwamba ilibidi wamalize tofauti zao kwa sababu ilikuwa kizingiti kwao kufanya muziki mzuri ambao walikuwa wakifanya miaka ya hapo nyuma.

Ikumbukwe mwaka wa 2017 Otile Brown alitengana na lebo ya  muziki ya dream land music chini ya uongozi wake Dr. Eddie, jambo  ambalo lilimfanya akawa msanii wa kujitegemea.

Kipindi hicho mkali huyo wa ngoma ya Dusuma, alisema kwamba kilichompelekea kutemana na lebo ya muziki ya Dream Land  ni kwa sababu Dr. Eddie alikwenda kinyume na mkataba wa maelewano.

Kitu ambacho kilimfanya Dr. Eddie kumzuia Otile Brown kutumia nyimbo alizorekodi chini ya lebo yake  ya muziki kwenye matamasha mbali mbali ya muziki. Lakini sasa inaonekana mambo yamekuwa mazuri, hivyo wawili hao wameahamu kufanya kazi tena.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa