EZEKIEL MUTUA AFUNGUKA SABABU ZA MULAMWAH KUTOPEWA WADHFA WA “CLEAN CONTENT AMBASSADORS”.”

You are currently viewing EZEKIEL MUTUA AFUNGUKA SABABU ZA MULAMWAH KUTOPEWA WADHFA WA “CLEAN CONTENT AMBASSADORS”.”
  • Post category:Burudani

Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu nchini  Ezekiel Mutua amefunguka na kueleza  sababu za  zilizopelekea mchekeshaji  wa humu nchini Mulamwah kutopewa  wadhfa wa  “Ubalozi wa Maudhui Safi” licha ya kuahidiwa wadhfa huo.

Kupitia ukurusa wake wa Twiter, Mutua amesema kuwa mcheshi huyo hakufikia vigezo vya kuwa “Balozi wa Maudhui Safi”, na ndio maana aliachwa nje huku akisema kuwa bodi hiyo haiungi mkono maadhui yanayokwenda kinyume na maadili ya jamii.

Mutua  alienda mbali zaidi na kuomba msamaha Mulamwah kwa kutoa ahadi hewa kwake ikizingatiwa kuwa maoni aliyoyatoa yalikuwa  mapendekezo yake binafsi wala hayakuwa ya serikali.

Kauli ya Mutua inakuja mara baada ya Mulamwah kuibua tweet yake ya zamani aliyomhaidi nafasi ya Ubalozi wa maudhui safi,ahadi aliyosema hajatimiza hadi sasa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa