OTILE BROWN AKOSELEWA KWA HATUA YA KUMTUMIA SHAKILLA KAMA VIDEO VIXEN KWENYE WIMBO WA “GO DOWN.”

You are currently viewing OTILE BROWN AKOSELEWA KWA HATUA YA KUMTUMIA SHAKILLA KAMA VIDEO VIXEN KWENYE WIMBO WA “GO DOWN.”
  • Post category:Burudani

Baadhi ya wadau wa muziki nchini wamemtolea uvivu Staa wa muziki nchini Otile Brown mara baada ya msanii huyo kumshirikisha mwanadada maarufu mitandaoni aitwaye Shakilla kwenye wimbo wake mpya uitwao “Go Down.”

Licha ya single hiyo kupokelewa kwa uzuri na wapenzi muziki mzuri nchini inaonekana  kuna baadhi ya watu ambao  hawajefurahishwa na  hatua ya Otile Brown kumtumia shakilla kama video vixen kwenye wimbo wake huo.

Sasa kupitia mitandao ya kijamii baadhi ya mashabiki wameonekana kumshambulia Otile Brown huku wakisema kwamba msanii huyo hakufanya vizuri kumshirikisha mrembo huyo kwenye wimbo wake wa “Go Down” kwani uwepo wake hauna mashiko kwenye  video ya wimbo huo.

Ikumbukwe tangu mwanadada Shakilla apate umaarufu nchini kupitia mitandao ya kijamii wakenya wengi hajewahi furahishwa na mienendo yake kutokana na vituko vyake ambavyo wengi wanahisi kwamba vinakwenda kinyume na maadili ya jamii.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa