HIGH SCHOOL ALBUM KUTOKA KWA HARMONIZE KUACHIWA RASMI MUDA WOWOTE.

You are currently viewing HIGH SCHOOL ALBUM KUTOKA KWA HARMONIZE KUACHIWA RASMI MUDA WOWOTE.
  • Post category:Burudani

Staa wa Muziki wa Bongofleva Harmonize ameendelea kutupasha mapya kuhusiana na ujio wa album yake mpya ambayo ameipa jina la HIGH SCHOOL. 

Akiwa kwenye moja ya interview wiki  hii, Harmonize amesema album hiyo tayari imekamilika kila kitu, anachosubiri ni kuona ratiba za wasanii wenzake kwenye label na kisha ataidondosha.

Kingine kikubwa ambacho Konde Boy amekifanya kwenye album yake hii ya Pili ni kutoshirikisha wasanii wa nje ya Tanzania, kama alivyofanya kwenye ‘Afro East’ ambayo ilisheheni majina mazito ya Afrika na dunia.

Harmonize amesema anataka kuwakaribisha watu kwenye Darasa lake na kuwaonesha sisi  kama Wana Afrika Mashariki tunaweza kufanya aina yoyote ya muziki. 

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa