T-PAIN “NINA MCHANGO MKUBWA KWA WASANII KUTUMIA AUTO-TUNE”

You are currently viewing T-PAIN “NINA MCHANGO MKUBWA KWA WASANII KUTUMIA  AUTO-TUNE”
  • Post category:Burudani

Sauti ya mwimbaji kutoka marekani T-Pain kwenye nyimbo zake ilikuwa tofauti na wasanii wengine kutokana na sauti yake kuwa ya kipekee, ambayo kitaalam inaitwa (auto-tune) ambayo ni effect maalum inayotumika kwenye studio za muziki.

Japo msanii huyo alipitia ukosoaji mkubwa kutoka kwa wasanii wengi nchini marekani akiwemo Jay-Z lakini hakukata tamaa kwenye shughuli zake za kimuziki.

Sasa mkali huyo wa ngoma”Bartender” ameibuka na kujinasibu kwamba wasanii wengi wa kisasa wanatumia auto-tune kuzinogesha nyimbo zao na yeye ndiye amewashawishi.

Kwenye mahojiano na Black Girl Nerds, T-Pain amesema kitendo cha wasanii kukumbatia auto tune inaonyesha ni jinsi gani walikuwa inspired na ubunifu wake.

“Kwa namna ilivyosambaa na namna ambavyo kila mmoja anaitumia kwa sasa, hiyo inanifanya nitambue kwamba nilikuwa nafanya kitu sahihi tangu awali. Kwa sababu kama ningekuwa sifanyi kitu sahihi, hakuna yeyote ambaye angefanya kwa sasa. Kwanini U-Copy kitu ambacho ni kibaya?” amesema T-Pain.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa