Kamanda wa polisi kaunti ya Trans-Nzoia Fredrick Ochieng’ ametangaza kuanza kwa oparesheni kali ya kuwanasa wale wote wanaokiuka sheria zilizowekwa na Wizara ya Afya kuzuia kuenea kwa virusi hatari wa Corona.
Ochieng’ amesema watawanasa wale wote ambao wamelegeza kanuni hizo wakiwemo wafanyibiashara wenye migahawa na vyumba vya burudani.
Ameongeza kwamba wamiliki wa magari hawatasazwa kwenye operesheni hiyo kwani wengi wao wamekuwa wakiuka masharti hayo licha ya inspekta