KUNDI LA WASOMI WA NAKWAMEKWI KUTOKA KAUNTI YA TURKANA LATOA MSAADA WA VYAKULA KWA WAKAAZI

Kundi la wasomi katika eneo la Nakwamekwi viungani mwa mji wa Lodwar wametoa msaada wa vyakula na bidhaa nyingine kwa  familia maskini ambazo zimeathirika pakubwa na janga la corona katika kijiji cha Nataparkakono.

Mwenyekiti wa kundi la wasomi wa Nakwamekwi Francis Nakwar amesema wamechukua hatua hiyo kuzisaidia familia 250 zisojiweza katika eneo hilo baada ya shughuli zao ambazo walikuwa wanategemea kama kitega uchumi kusimamishwa kutoka na corona.

Aidha amesema wametumia hafla hiyo kutoa elimu kwa wakaazi kuhusu umuhimu wa kujikinga na virusi vya COVID-19 kwa kuosha mikono kila mara wakitumia maji tiririka na sabuni pamoja vitakasa.

Wakati uo huo wamewataka wananchi  kuachana mila na desturi zitakazochangia kuenea kwa ugonjwa  wa corona endapo utaingia kaunti hiyo huku wakitoa wito kwa serikali ya kaunti kusambaza maji katika eneo hilo ili kupiga jeki mapambano dhidi ya corona.

Hata hivyo wametoa wito kwa serikali kuu,ya kaunti na mashariki mengine ya kijamii kutoa msaada wa vyakula kwa wakaazi wa kaunti ya Turkana ambao wameathirika na janga la corona.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa