OMAH LAY ADAI KUIBIWA VITU VYAKE AKIWA UWANJA WA NDEGE.

You are currently viewing OMAH LAY ADAI KUIBIWA VITU VYAKE AKIWA UWANJA WA NDEGE.
  • Post category:Burudani

Mwimbaji kutoka nchini Nigeria Omah Lay ameweka wazi kuibiwa vitu vyake akiwa uwanja wa ndege huku msanii huyo akiwa anajiuliza kama waliomuibia vitu hivyo walikuwa wanataka nyimbo zake ambazo hazijatoka au kitu gani.

Omah Lay ametoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa Twitter kwa kuandika “Nimeibiwa laptop,Microphone na Audio interface kutoka kwenye box langu uwanja wa ndege,nyinyi watu mlikuwa mnatafuta hit song au kitu gani?”

Omah Lay hajaweka wazi moja kwa moja ni uwanja gani wa ndege ambao ameibiwa vitu hivyo lakini pia hajaweka wazi tukio hilo lilitokea lini.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa