JOSE CHAMELEONE ADAI UCHAGUZI ULIOPITA WA UMEYA KAMPALA ULIKUMBWA NA DOSARI NYINGI.

You are currently viewing JOSE CHAMELEONE ADAI UCHAGUZI ULIOPITA WA UMEYA KAMPALA ULIKUMBWA NA DOSARI NYINGI.
  • Post category:Burudani

Msanii nguli wa muziki kutoka nchini Uganda Jose Chameolene amedai kwamba kura zake kwenye kinyanganyiro cha umeya wa jiji la Kampala zilikumbwa na dosari nyingi.

Akiwa kwenye moja ya Interview Chameleone amesema kura zake ziliaharibiwa na baadhi ya wagombea waliojitokeza kuwania wadhfa huo ambao waliogopa umaarufu wake.

Hata hivyo amedokeza mpango wa kurejea tena kwenye kiwanda cha  muziki nchini Uganda kwa kishindo lakini pia amedai kwamba ataelekeza nguvu zake zote kuboresha kituo chake cha runinga kiitwacho Leone Island TV.

Ikumbukwe Jose Chameolene alipoteza kwenye uchaguzi wa umeya wa jiji la Kampala mapema mwaka huu na mpinzani wake Erias Lukwago.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa