MWANADADA ELSIE MAJIMBO AKAVA JARIDA LA TEEN VOGUE LA NCHINI MAREKANI.

You are currently viewing MWANADADA ELSIE MAJIMBO AKAVA JARIDA LA TEEN VOGUE LA NCHINI MAREKANI.
  • Post category:Burudani

Mchekeshaji wa humu nchini  Elsie Majimbo  amekava Jarida la Teen Vogue  toleo la mwezi machi mwaka huu.

Majimbo ambaye yupo nchini mMarekani kwa sasa hakuficha furaha yake kwani alitumia mitandao yake ya kijamii kwa hatua hiyo kubwa maishani huku akimshukuru mungu kwa kumpigania licha ya watu kwenye mitandao kumbeza.

Kwa matokeo hayo, baadhi ya wafuasi wake kwenye mitandao ya kijamii wameonekana kufurahia  mafanikio aliyoyapata ambapo wengi wampongeza mrembo huyo kwa hatua hiyo kubwa maishani kwani sio jambo rahisi kwa   mtu kutoka afrika kukava jarida la Teen Vogue.

Ikumbukwe Jarida la teen vogue ni jarida ambalo hutoka mara 12 kwa mwaka yaani mara moja kila mwezi na husisha watu mashuhuri pamoja na tasnia ya mitindo na Fasheni.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa