Staa wa muziki nchini Mejja amejibu tuhuma zilizoibuliwa na aliyekuwa member wa kundi la Kansoul, Kid Kora.
Akiwa kwenye moja ya Interview Mejja amekanusha madai ya kumtumia vibaya Kid Kora huku akisema kwamba msanii huyo alikuwa anapenda sana kuishi maisha ya starehe, kitendo ambacho kilimpelekea kushindwa na shughuli za muziki.
Aidha amesema kwamba ni yeye na Madtraxx ndio walihamua kujitenga na Kid Kora kwa sababu alikuwa kizingiti kwa maendeleo ya kundi la Kansoul kimuziki.
Kauli ya Mejja inakuja mara baada ya Kid Kora kudai kuwa alijiondoa kwenye kundi la Kansoul kwa sababu hakufaidi na chochote kwani member wenzake Mejja na Madtraxx walivyonza pesa zote za nyimbo zao.