“MTV BASE AFRICA” WAAHIRISHA UTOAJI WA TUZO

You are currently viewing “MTV BASE AFRICA” WAAHIRISHA UTOAJI WA TUZO
  • Post category:Burudani

Waandaaji wa tuzo za MTV Africa Music Awards wameahirisha hafla za ugawaji wa tuzo hizo zilizokuwa zifanyike Kampala Uganda Februari 20 mwaka huu.

Kwenye taarifa yao, MTV Base wamesema wameahirisha ugawaji wa tuzo hizo za 7 mpaka itakapotangazwa tena huku wakishindwa kutaja sababu iliyopolekea kuahirishwa kwa tuzo hizo.

Tovuti ya CCN imeripoti kwamba Bobi Wine na wafuasi wake wanahusika kwenye sababu za MTV MAMA kuahirishwa kutokana na madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na serikali ya Uganda, madai ambayo yamewasilishwa mtandaoni na Bobi Wine ambaye alikuwa mgombea wa kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa