NICAH THE QUEEN ANYOSHA MAELEZO KUHUSU VIDEO YAKE ILIYOKUWA IKISAMBAA MITANDAONI.

You are currently viewing NICAH THE QUEEN ANYOSHA MAELEZO KUHUSU VIDEO YAKE ILIYOKUWA IKISAMBAA MITANDAONI.
  • Post category:Burudani

Mwanamuziki wa nyimbo za injili nchini Nicah the Queenn amenyosha maelezo kuhusu video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha akijaribu kuwaalika watu  kanisani wikiendi iliyopita.

Kupitia Insta story yake kwenye mtandao wa Instagram Nicah amesema hakutegemea video hiyo itatrend kwani aliitengeneza bila kukusudia lakini kwa bahati mbaya alishangaa imetrend kwa sababu ya maungo yake ya mwili.

Mkali huyo wa ngoma ya “Ushuhuda” amedai kwamba mwili wake haufai kutambulisha dini lake  au kueleza upendo wake kwa Yesu kristo kwani hata akivalia gunia makalio yake yataonekana tu.

Kauli ya Nicah the Queen inakuja mara baada ya Wakenya kwenye mitandao ya kijamii kumtolea uvivu msanii huyo kwa madai ya kuchapisha video hiyo kwa kukusudia ili kuonyesha maungo ya mwili wake huku akiwasilisha ujumbe wa kanisa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa