Nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania Ibraah yuko jikoni kwa ajili ya kuiandaa album yake ya kwanza tangu aanze safari yake ya muziki.
Kupitia Instastory yake kwenye mtandao wa instagram meneja wa lebo ya muziki ya konde gang Mjerumani amepost picha ya ibraah akiwa studio na kuandika “Blessed son album n the making”.
Kama album hiyo itatoka itakuwa ni album ya kwanza kwa msanii huyo ambaye tayari alifanikiwa kuachia “EP” yake inayofahamika kama “Steps” iliyotoka mwaka 2020 .
Sanjari na hilo Ibraah amewaacha mashabiki zake na maswali baada ya kupost picha akiwa na mwanamke wa kizungu bila kuandika chochote.
Watu wengi wanadhani huenda akwa ndiye mpenzi wake mpya kutokana na comments za wanafamilia wenzake wa lebo ya konde gang.