MCHEZO WA SOKA KATI YA WATANI WA JADI GOR MAHIA NA FC LEOPARDS KUPIGWA BILA MASHABIKI KESHO

You are currently viewing MCHEZO WA SOKA KATI YA WATANI WA JADI GOR MAHIA NA FC LEOPARDS KUPIGWA BILA MASHABIKI KESHO
  • Post category:Michezo

Mabingwa watetezi wa Ligi kuu nchini Gor Mahia watashuka uwanjani Kasarani Jumapili  Februari 7  kwa mechi ya ligi kuu maarufu kama Mashemeji Derby huku kwa mara ya kwanza mechi ya hiyo ya ubabe na utani mkubwa ikichezwa bila mashabiki uwanjani kutoka na ugonjwa wa Covid 19.

Timu zote mbili zilikuwa zimewasilisha ombi kwa wizara ya afya  kuruhusu angalau mashabiki 5,000 ila ombi hilo lilikataliwa na  kuwalazimu mashabiki kusalia nyumbani wakati wa mchuano huo siku ya  Jumapili .

Klabu ya FC Leopards ni ya 4 kwenye msimamo wa ligi nchini kwa pointi 18 wakati Gor Mahia ikishikilia nafasi ya 6 kwa alama 15.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa