MAREKANI YASEMA MWANAMFALME WA SAUDI ARABIA ALIHUSIKA NA MAUAJI YA JAMAL KHASHOGGI.

You are currently viewing MAREKANI YASEMA MWANAMFALME WA SAUDI ARABIA ALIHUSIKA NA MAUAJI YA JAMAL KHASHOGGI.

Ripoti ya Intelijensia ya Marekani imesema Mwanamfalme wa Saudi, Mohammed bin Salman aliidhinisha mauaji ya Mwandishi wa Habari Jamal Khashoggi yaliyotokea mwaka 2018.

Kwa mujibu wa Ripoti hiyo iliyotolewa chini ya Utawala wa Rais Joe Biden, imeelezwa Mwanamfalme alipitisha mpango wa kumkamata au kumuua Mwanahabari huyo. Khashoggi aliuawa ndani ya Ubalozi wa Saudi Arabia Mjini Istanbul, Uturuki.

Marekani imetangaza vikwazo dhidi ya watu mbalimbali Saudi Arabia isipokuwa Mwanamfalme Salman. Saudi Arabia imepinga Ripoti hiyo ikisema ni ya uongo na haikubaliki.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa