MYANMAR: BALOZI AFUTWA KAZI BAADA YA KUHIMIZA JESHI KUONDOLEWA MADARAKANI.

You are currently viewing MYANMAR: BALOZI AFUTWA KAZI BAADA YA KUHIMIZA JESHI KUONDOLEWA MADARAKANI.

Watawala wa Jeshi Nchini Myanmar wamemfuta kazi Balozi wa Taifa hilo wa Umoja wa Mataifa (UN) ikiwa ni siku moja baada ya kauli yake ya kuomba msaada ili Jeshi liondolewe madarakani.

Katika hotuba yake, Kyaw Moe Tun alisema watu wote wasishirikiana na Jeshi mpaka madaraka yatakaporejeshwa kwa Serikali iliyochaguliwa kidemokrasia.

Vilevile, Balozi huyo alitoa wito kwa jamii ya kimataifa kutumia mbinu zozote kuchukua hatua dhidi ya Jeshi ili kusaidia kurejesha Demokrasia, akisema anawakilisha Serikali ya Aung San Suu Kyi iliyotolewa madarakani.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa