KUNDI LA OCHUNGULO FAMILY LAVUNJIKA HUKU NYIMBO ZAO ZOTE ZIKIFUTWA YOUTUBE.

You are currently viewing KUNDI LA OCHUNGULO FAMILY LAVUNJIKA HUKU NYIMBO ZAO ZOTE ZIKIFUTWA YOUTUBE.
  • Post category:Burudani

Kundi la muziki wa Gengetone nchini Ochungulo Family limevunjika baada ya kwa nyimbo zao zote kufutwa kwenye mtandao wa Youtube.

Taarifa za kundi hilo kuvunjika zilianza kusambaa mitandaoni jumatano wiki hii wakati akaunti yao ya youtube yenye wafuasi elfu 158 ilichukuliwa na Nelly The Goon ambaye ni mmoja kati ya members wa Ochungulo Family.

Kundi la Ochungulo Family ambalo lilikuwa linaundwa na wasanii Benzema, Nelly The Goon na Dmore halijeweka wazi sababu za kuafikia uamuzi huo ila wajuzi wa mambo wanahisi kwamba huenda wasanii wa kundi hilo wamekuwa na mgogoro wa kugawa mapato na ndio chanzo cha kuvunjika kwake.

Ikumbukwe wasanii wa Ochungulo Family wamekuwa wakifanya kazi kama wasanii wa kujitegemea huku wakishirikishwa na wasanii kwenye kazi zao kabla ya kuafikia uamuzi wa kulivunja kundi hilo.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa