KRG THE DON AMCHANA BENZEMA BAADA YA KUNDI LA OCHUNGULO FAMILY KUVUNJIKA.

You are currently viewing KRG THE DON AMCHANA BENZEMA BAADA YA KUNDI LA OCHUNGULO FAMILY KUVUNJIKA.
  • Post category:Burudani

Msaniii wa muziki nchini KRG the Don amemtolea uvivu msanii mwenzake Benzema aliyekuwa anaunda kundi la Ochungulo family ambalo lilivunjika majuzi.

Kupitia ukurasa wake wa instagram mkali huyo wa  ngoma ya “Giddem” amempongeza wasanii Nelly the Goon na DMore kwa hatua ya kujitenga na Benzema ambaye alikuwa member wa kundi hilo akisema kuwa msanii huyo sio mtu mzuri ikija kwenye masuala ya biashara kwani ni tapeli.

Kauli hiyo ya Krg the Don haikupokelewa vyema na wadau wa muziki nchini ambao wamemchana msanii huyo akome kutumia lugha ya matusi kwa wasanii wengine ikizingatiwa kuwa hana idhibati ya kuonyesha Benzema ni tapeli.

Ikumbukwe KRG The Don hana uhusiano mzuri na Benzema tangu alipoibua madai kwamba Benzema alivuja pesa za miraba au royalties ya  wimbo wao uitwao “Doremi” mwaka wa 2020.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa