KID KORA AFUNGUKA SABABU ZA KUJIONDOA KWENYE KUNDI LA KANSOUL.

You are currently viewing KID KORA AFUNGUKA SABABU ZA KUJIONDOA KWENYE KUNDI LA KANSOUL.
  • Post category:Burudani

Aliyekuwa member wa kundi la Kansoul, Kid Kora amefunguka kwa mara ya kwanza sababu za kujiondoa kwenye kundi hilo miaka minne iliyopita.

Kora ambaye aliacha kutumia jina “Kid” kwenye shughuli zake za kimuziki amedai kwamba members wenzake ambao ni Mejja na Madtraxx walikuwa wanamtumia vibaya lakini pia walimzuia kufaidi na miraba au royalties ya nyimbo zao.

Kora alienda mbali sana na kuwachana members wenzake Mejja na Madtraxx  kwa hatua ya kukataa kubadilisha maudhui ya nyimbo zao ambayo amedai kwamba ilikuwa inawavunjia wanawake heshima.

Ikumbukwe Rapa huyo mwenye umri wa miaka 34 amekuwa na kundi la Kansoul kwa miaka saba kabla ya kujiondoa mwaka wa 2018 na tangu kipindi hicho hakutoa sababu ya kujitenga kwake.

Mejja,Madtraxx na Kora walipata mafanikio makubwa kama kundi la Kansoul kwani licha ya kuachia singles kali walifanikiwa pia kuteuliwa kushiriki kwenye tuzo za MTV Africa Music kupitia kipingele cha Listeners Choice. 

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa