ERIC OMONDI AMUOMBA RADHI “C.E.O” WA “KFCB” DR. EZEKIEL MUTUA.

You are currently viewing ERIC OMONDI AMUOMBA RADHI “C.E.O” WA “KFCB” DR. EZEKIEL MUTUA.
  • Post category:Burudani

Mchekeshaji maarufu nchini Eric Omondi amemuomba msamaha Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Uainishaji wa Filamu nchini Ezekiel Mutua.

Eric amethibitisha kuomba msamaha kupitia akaunti yake ya Instagram baada ya kuachiliwa kwa dhamana ya shilingi elfu 50 jana, siku moja baada ya kukamatwa kwa makosa ya jinai.

Mchekeshaji huyo alikamatwa Machi 11  mwaka huu kwa kukiuka sheria ya maadili katika utengenezaji na maonyesho ya filamu kwa kipindi chake cha ‘Wife Material’.

Eric omondi amekubaliana na Mutua baada ya kufanya naye mazungumzo kwa njia ya simu kuwa kipindi chake hicho hakihitaji kuwa na mahudhui yasiyofaa ili kupata wafatiliaji.

Pia Eric omondi amewaomba radhi watu wote aliowakwaza kwa namna yoyote kupitia kipindi chake hicho alichokitaja kuwa anakitumia kuiunganisha Afrika mashariki kupitia Burudani.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa