KAUNTI YA TRANS-NZOIA YAZINDUA ZOEZI LA KUTOA CHANJO YA CORONA KWA WAHUDUMU WA AFYA NA MAKUNDI MINGINE MAALUM

You are currently viewing KAUNTI YA TRANS-NZOIA YAZINDUA ZOEZI LA KUTOA CHANJO YA CORONA KWA WAHUDUMU WA AFYA NA MAKUNDI MINGINE MAALUM

Wizara ya afya katika kaunti ya Trans-Nzoia imeanza mpango wa kuwapa chanjo ya COVID-19 wahudumu wa afya,

Hii ni baada ya kaunti hiyo kupokea dozi 6000 chanjo hiyo, katika mpango ambao pia unawalenga maafisa wa usalama.  

Akipokea chanjo hiyo gavana Patrick Khaemba amedokeza kwamba serikali yake itahakikisha kwamba wanaohitaji  chanjo hiyo wanapata ili kukabili kuenea kwa maradhi ya COVID-19.

Kwa upande wake kamishna wa kaunti ya Trans-Nzoia Sam Ojwang amewaonya wananchi ambao wanaendelea kupuuza masharti yaliyowekwa kukabili Corona akisema watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa