Kim Kardashian na rapa Kanye West kutoka nchini Marekani wamegawana mali kufuatia kuvunjika kwa ndoa yao mara baada ya Kim kudai talaka.
Sasa imearifiwa kwamba Kim Kardashian atabaki na nyumba iliyopo Hidden Hills mjini California.
Wawili hao walilipa kiasi cha shillingi billioni 2.1 kununua nyumba hiyo mwaka 2014 baada ya kufunga ndoa na walitumia kiasi kama hicho tena kuiboresha.
Kim amelazimika kuchukua nyumba hiyo kwa ajili ya malezi ya watoto wao. Lakini pia familia yake inahisiwa kuchochea Kim abaki mitaa hiyo kwa sababu na wao wanaishi huko.
Kwa kipindi cha hivi karibuni Kanye West amekuwa akiishi Wayoming kwenye eneo ambalo alilinunua mwaka wa 2019.