KAMPUNI YA NICKELODEON YATOA ORODHA YA WATU WANAOWANIA TUZO ZA NICKELODEON KIDS CHOICE AWARDS 2021.

You are currently viewing KAMPUNI YA NICKELODEON YATOA ORODHA YA WATU WANAOWANIA TUZO ZA NICKELODEON KIDS CHOICE AWARDS 2021.
  • Post category:Burudani

Kampuni ya Nickelodeon imeweka orodha ya majina ya watu walioteuliwa kuwania tuzo za Nickelodeon Kids Choice Awards mwaka 2021.

Mchekeshaji mdogo wa kike kutoka nchini Nigeria, emanuella, mwanadada Elsie Majimbo wa humu nchini na vijana kutoka nchini Uganda Ghetto Kids  ni miongoni mwa waliochaguliwa kuwania tuzo hizo mwaka huu.

Orodha ya washiriki wa kuwania tuzo za Nickelodeon Kids Choice Awards  mwaka 2021 imewekwa wazi na kampuni hiyo kupitia tovuti yao ambapo tayari watu wameanza kupiga kura kupitia tovuti hiyo hiyo KidsChoiceAwards.com

Tuzo hizo zitatolewa ifikapo Machi 13, na zoezi zima litaonyeshwa katika channel za waandaji wa tuzo hizo pamoja na programu ya matangazo ya moja kwa moja katika vifaa vya iPad, iPhone, na Android kwa wakazi wa nchini Marekani.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa