BOW WOW KUJIKITA KWENYE MCHEZO WA MIELEKA BAADA YA KUACHA MUZIKI.

You are currently viewing BOW WOW KUJIKITA KWENYE MCHEZO WA MIELEKA BAADA YA KUACHA MUZIKI.
  • Post category:Burudani

Staa wa muziki kutoka nchini Marekani Bow Wow ametangaza vitu ambavyo atajikita navyo baada ya kuachana na muziki. 

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter rapa huyo amesema atajikita kwenye utengenezaji filamu na vipindi vya televisheni lakini pia atajiunga na mchezo wa Mieleka maarufu kama Wrestling chini ya kampuni ya WWE.

Aidha ameenda mbali zaidi na kumtaja mwana masumbwi Rey Misterio kuwa mshirika wake kisha akasema yupo tayari kushindana na yeyote yule kuwania mkanda wa Tag Team.

Bow Wow  ni rapa,mwigizaji na mtangazaji kutoka nchini marekani na alianza kujihusisha na mambo ya muziki mwaka wa 1993 na mpaka sasa  ana album zaidi ya 15 tangu aanze muziki.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa