AKOTHEE “NAOGOPA UJAZITO KULIKO CORONA.”

You are currently viewing AKOTHEE “NAOGOPA UJAZITO KULIKO CORONA.”
  • Post category:Burudani

Staa wa muziki nchini Esther Akoth maarufu kama Akothee amesema kuwa anaogopa kupata Uja Uzito kuliko virusi vya Covid-19 kwa sababu tu wanaume wa siku hizi hawatoi matunzo kwa watoto wao.

Kauli hiyo inakuja mara baada ya kuwadanganya wafuasi wake na uchunguzi bandia wa ujauzito,huku akisisitiza kuwa yeye ni mjamzito.

Aidha ametoa wito kwa mashabiki wake wamruhusu aendelee kuota ndoto ya kupata ujauzito, bila ya kuifanya iwe kweli.

Mwanamuziki huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo wake uitwao Dende Yom amekuwa akizungumzia suala la kupata mtoto kwa muda sasa ambapo mwezi Agosti mwaka jana, alikuwa na tamaa ya kupata mtoto wa sita.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa